Manchester United wakiwa ugenini huko Hisapania wamelazimisha sare ya 1-1 ugenini mbele ya Atletico Madrid katika mchezo wa mkondo wa kwanza hatua ya 16 bora ligi ya Mabingwa Barani Ulaya.
Joao Felix alianza kuifungia Atletico mapema dakika ya 7, kipindi cha kwanza kabla ya Anthony Elanga kuja kuisawazishia United katika dakika ya 80 kipindi cha pili.
Timu hizo zitarudiana majuma mawili yajayo kuamua hatma ya timu itakayosonga mbele katika hatua ya robo fainali ya michuano hiyo mikubwa kwa ngazi ya vilabu Ulaya.
Katika mechi nyingine ya Ligi hiyo, Benfica naye ametoa sare ya bao 2 - 2 na Ajax.