Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

UCHAMBUZI: Kaze keshaijua ramani, hawezi kupotea kizembe

Kaze Pic Data UCHAMBUZI: Kaze keshaijua ramani, hawezi kupotea kizembe

Mon, 1 Mar 2021 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

HUENDA mechi tatu ambazo Yanga ilipata sare mfululizo, zilitosha kumnyoosha Cedric Kaze. Ndio, mechi ya kwanza ilikuwa dhidi ya Tanzania Prisons kabla ya Ligi Kuu Bara.

Hii haikufuatiliwa sana, lakini ligi iliporejea tena na Yanga ililazimishwa sare ya 1-1 dhidi ya Mbeya City.

Mechi hii iliwashtua wanayanga. Naweza kusema hapa mambo yalitibuka Jangwani. Lakini wanayanga walichefukwa zaidi, pale walipoishuhudia timu yao ikitoka sare ya mabao 3-3 na Kagera Sugar.

Tena ikiwa nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa. Katika mechi ambayo walipotea mno hasa kipindi cha kwanza. Kitendo cha Kaze kumuanzisha benchi Mukoko Tonombe na kusababisha timu kupwaya iliwakata stimu mashabiki wa klabu hiyo. Sura zao zilionyesha hivyo mbele ya kamera za Azam TV.

Hawakujua nini kinaenda kutoka kwa timu yao. Bahati nzuri kipindi cha pili, Kaze alimrejesha kikosini Mukoko. Kiungo huyo fundi, aliirejesha Yanga mchezoni na kupata sare hiyo ya 3-3.

Utabisha nini hizo ni mechi ambazo zilimnyima raha Kaze? Hii ni kutokama na masimango kutoka kila kona ya nchi. Wananchi walichefukwa. Kama utakuwa unabisha kwa hiki ninachokisema, angalia tu namna alivyoshangilia bao la Carlinhos walipoinyoa Mtibwa Sugar katika mchezo uliofuta. Kama hiyo unaikataa basi isikilize upya kauli alizotoa kwenye mkutano wake na wanahabari baada ya mechi dhidi yas Mtibwa. Alishindwa kuficha hisia zake, namna alivyoumizwa na maneno yaliyokuwa yakielekezwa kwake na hata kwa timu yake. Aliumizwa na watu aliowaita wachambuzi. Uzuri tu, kocha huyo Mrundi hakuvuka mipaka katika kueleza alivyoumizwa na masimango hayo, ila ilitosha kuonyesha amepata somo. Hata mwenyewe alikiri, ameelewa tamaduni za wadau wa soka nchini. Amewajua kiundani Wanayanga walivyo, hasa timu yao inapopata matokeo ya ovyo. Wahenga wanasema fimbo ikuchapato ndiyo ikufunzayo! Kajifunza!

Chanzo: mwanaspoti.co.tz