Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

UBISHI WA MZEE WA KALIUA: Kuna dhambi yoyote Yanga ikikosa ubingwa?

Pic Kaze Data UBISHI WA MZEE WA KALIUA: Kuna dhambi yoyote Yanga ikikosa ubingwa?

Thu, 25 Feb 2021 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

Kosa kubwa la Klabu ya Yanga ni kutaka kuwa na uwezo kama wa Simba kwa msimu mmoja tu! Simba haipo hapo kwa Bahati mbaya, wamewekeza sana kwa wachezaji, benchi la Ufundi, huduma za uhakika na kwa muda mrefu.

Yanga inaweza kuwa Bingwa msimu huu na hakuna tatizo. Yanga inaweza isiwe Bingwa na hakuna tatizo pia.

Ufalme walionao Simba kwa sasa ndani ya Ligi Kuu Tanzania Bara, waliusubiri kwa misimu mitano. Walijipanga, walivumilia, waliumia lakini mwisho wamejenga timu imara.

Tangu msimu wa 2012/2013 hadi 2017/208, Simba alikuwa anatazama michuano ya Vilabu Afrika kwenye Runinga tu! Ndiyo mpira ulivyo wakati mwingine! Simba hakushiriki michuano ama ya Klabu Bingwa au Kombe la Shirikisho Afrika kwa miaka mitano mfululizo na haikuwa dhambi.

Kuna kosa kubwa moja viongozi wa Yanga walilifanya tangu mwanzo wa msimu huu, unakumbuka? Ngoja nikukumbushe.

Walisikika mara nyingi wakisema kwamba msimu huu Ubingwa unaenda Jangwani! Hii ahadi ndiyo inayowatesa kwa sasa. Hii ndiyo ahadi inayoleta presha kubwa sana kwa sasa kwa Wachezaji, Benchi la Ufundi, Viongozi na Mfadhili wao! Yanga wana timu Bora sana msimu huu kuliko misimu mitatu iliyopita lakini bado hawajafikia ubora walionao Simba kwa sasa.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz