Thu, 21 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya taifa ya wanawake ya Tanzania, Twiga Stars imeondoka Dar es Salaam Jumatano usiku kwenda Afrika Kusini kwa ajili ya mchezo wa marudiano na Namibia Jumamosi Uwanja wa Dobsonville Jijini Johannesburg Raundi ya Kwanza kufuzu AFCON ya mwakani Morocco.
Twiga Stars imeondoka mara tu baada ya kuchapwa mabao 2-1 na Namibia nyumbani Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam jioni ya Jumatano.
Mchezo wa marudiano kufuzu AFCON dhidi ya Namibia utakaochezwa Oktoba 23, 2021 uwanja wa Dobsonville, Soweto, Afrika ya Kusini.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live