Fri, 13 Aug 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Tanzania ya Wanawake (Twiga Stars) imepangwa Kundi B katika michuano ya Kombe la Mataifa ya Kusini mwa Afrika kwa Wanawake, ijulikanayo kama COSAFA Cup 2021.
Katika michuano hiyo, Twiga Stars imewekwa kundi moja na Botswana, Sudan Kusini na Zimbabwe.
Kundi A kuna wenyeji, Afrika Kusini, Angola, Malawi na Msumbiji na Kundi C zipo Zambia, Namibia, Eswatini na Uganda.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live