Timu ya Taifa ya Wanawake 'Twiga Stars' leo itakamilisha mechi za hatua ya makundi za michuano ya Cosafa inayoendelea nchini Afrika Kusini kwa kucheza na Sudani Kusini.
Kocha Mkuu wa timu hiyo Bakari Shime, amesema maandalizi ya mchezo huo unaotarajiwa kuanza majira ya saa 7: 00 kwa saa za Tanzania yamekamilika na matumaini yao ni kushinda mchezo huo.
"Maandalizi yetu kuelekea mchezo huo yamekamilika kwa asilimia zote wachezaji wangu wote wapo katika hali nzuri na lengo letu ni kushinda ili kumaliza vinara kwenye kundi B, " amesema Shime
Twiga Stars inayoshiriki michuano hiyo kama timu mwalikwa mpaka sasa imecheza mechi mbili dhidi ya Zimbabwe na Botswana na kushinda zote na kocha Shime amesema lengo lao ni kurudi na Kombe hilo.