Fri, 22 Oct 2021
Chanzo: globalpublishers.co.tz
Kocha wa Timu ya Taifa ya Wanawake, Twiga Stars, Bakari Shime, amesema walifanya makosa kwenye mchezo uliopita wakiwa nyumbani na sasa wanakwenda kuwafunga Namibia wakiwa kwao, kesho Jumamosi.
Twiga Stars walichapwa 2-1 na Namibia kwenye mchezo wa kusaka tiketi ya kwenda Afcon mwakani, kwenye mtanange uliochezwa juzi Jumatano Uwanja wa Mkapa, Dar.
Akizungumza na Championi Ijumaa, Shime amesema walifanya makosa kwenye mchezo uliopita, wameliona hilo na watakwenda kulifanyia kazi wakiwa ugenini ambako kwa namna yoyote lazima wapate ushindi.
Chanzo: globalpublishers.co.tz