Thu, 26 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi chaTwiga Stars leo kinashuka dimbani kusaka tiketi ya kufuzu mashindano ya Olimpiki.
Kocha mkuu wa timu hiyo, Bakari Shime, amesema wanahitaji ushindi katika mchezo huo ili kujihakikishia nafasi.
Tanzania itakuwa mwenyeji wa mchezo huo wa hatua ya pili dhidi ya Botswana kuwania kufuzu Olimpiki mwakani nchini Ufaransa, mchezo utakaochezwa kuanzia saa 10.00 jioni katika Uwanja wa Azam Complex.
Shime alisema amekaa na wachezaji wake kuwaandaa kimbinu na kisaikolojia ili kuweza kutumia vyema uwanja wao wa nyumbani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live