Sat, 17 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Taarifa kutoka baadhi ya vyombo nchini Ufaransa na marafiki wa karibu wa Karim Benzema wanadai kuwa, Kocha wa Ufaransa Didier Deschamps alichukizwa na kitendo cha Benzema kutomshukuru wakati ametwaa Ballon dor zaidi ya kumtaja Zinadine Zidane.
Imeenda mbali zaidi na kusemekana kuwa Kocha amegoma kumwita Benzema kambini kuelekea fainali kutokana na sababu hizo, huku jana kupitia Instastory ya Rafiki wa karibu wa Benzema anaitwa Big Ben ameandika:
“Benzema ni Mchezaji bora duniani” huku akisindikiza na bendera ya Algeria ambalo ni taifa la asili la Karim"
Chanzo: www.tanzaniaweb.live