Sun, 27 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nafikiri tutakuwa tunamnyima Max haki yake kama hatutozungumzia kitu kimoja, akili yake (IQ) ya mpira + uwezo wa kuongeza kasi ya mchezo.
Kama wenzie wataweza kumsoma akiwa na mpira akiwa anaangalia mbele huku akiongeza kasi basi wataweza kuingia kwenye maeneo mazuri kwa haraka.
Max akianza tu kuongeza kasi basi kuna mpira wenye madhara unapigwa sehemu.
Kwa kumtazama tu nadhani bado hajafikia katika ubora wake asima miamoja, na itakapofika hapo tutakuwa tuna hadithi nyingine tofauti.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: