Baada ya kuliona kundi letu F la AFCON ya mwakani pale nchini Ivory Coast,nadhani nafasi yetu naiona kupitia wale BEST LOOSER wanne.
Makundi yapo 6 na kila kundi litatoa timu mbili za juu ambazo zitakwenda 16 bora ambapo jumla zitakuwa timu 12,hivyo nafasi yetu Tanzania tunaweza kuipata katika zile timu 4 ili kukamilisha timu 16.
Kiuhalisia Morocco wametuacha mbali,kama tunaweza labda kupata sare kwao,hawa DRC Congo na Zambia mmoja hapa tunapaswa kumfunga ili angalau tukimaliza na alama 4 basi tupate BEST LOOSER.
Hawa Zambia na DRC Congo mara nyingi tunacheza nao na huwa tunafahamiana sana,hapa ndio ilipo nafasi yetu. Vinginevyo tukiwashindwa Zambia na DRC Congo basi tutakuwa washiriki.