Wananchi Yanga SC wametamba kwamba kesho ndio siku yao ya kumshusha tembo kileleni kwenye msimamo wa Ligi Kuu ya NBC.
Isikupe tabu licha ya kuwa hajaweka wazi kuhusu tembo ni nani lakini ni dhahiri shahiri, tembo atakuwa ni Simba SC ambaye ndiye yupo kileleni kwenye msimamo kwa sasa baada ya kucheza mechi mbili za Ligi Kuu.
"Kesho Wanayanga tujitokeze kwa wingi tunataka kumshusha tembo pale alipo ili sisi tukae mahali petu," alisema Kamwe.
Yanga wapo nafasi ya nne kwenye msimamo wakiwa wamecheza mechi moja tu ya Ligi Kuu dhidi KMC na kuibuka na ushindi wa goli 5-0.
Kesho anakwenda tena kuzisaka alama tatu dhidi maafande wa JKT Tanzania ambao wamepanda Ligi Kuu msimu huu. Mechi yao ya kwanza dhidi ya Namungo, JKT walishinda kwa goli 1-0 wakiwa ugenini.