Tue, 27 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, amesema klabu yao kuingia hatua ya Robo Fainali Klabu Bingwa wameshazoea tofauti na watani wao YangaSC.
Amesema kwao ni vitu vya kawaida tofauti na watani zao ambao wameshangilia sana baada ya juzi kufuzu kwa kuwafunga CR Belouzdad.
“Yanga wanashangilia sana kuingia Robo fainali lakini sisi ni maisha yetu haya na tumeshazoea, tunawakaribisha kwenye huu ulimwengu wetu,” alisema Ahmed.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live