Fri, 10 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mchambuzi wa soka Musa Mwakisu amesema, kashfa ya baadhi ya wachezaji kudaiwa kuuza mechi imewasababisha wachezaji wa Simba SC kucheza chini ya kiwango dhidi ya Namungo FC.
Simba waliokuwa wenyeji kwenye mchezo wa raundi ya tisa ya Ligi Kuu ya NBC, walilazimika kupata sare ya 1-1 baada kutanguliwa kufungwa.
"Wachezaji walikuwa na siku mbaya sana mchezoni jana, ni kama vile walikuwa wameathiriwa kisaikolojia na suala la kuuza mechi dhidi ya Yanga, mchezo wa mpira unachezwa kuanzia kichwani, wao hawakuwa sawa," alisema Mwakisu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live