Sun, 24 Dec 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Meneja wa ‘klabu’ ya Liverpool, Jurgen Klopp amethibitisha kuwa beki wao Kostas Tsimikas atakuwa nje ya uwanja kwa muda mrefu baada ya kugongwa kwenye bega na winga wa ‘klabu’ ya Arsenal, Bukayo Saka dakika ya 35 kwenye sare ya 1-1 dhidi ya Arsenal siku ya jana.
Inaelezwa kuwa hilo siyo pigo la kwanza katika klabu hiyo, beki wa kushoto Andy Robertson pia yupo nje kwa sasa kutokana na jeraha la bega.
Hata hivyo, Bukayo amemuomba msamaha kwa rafu yake iliyopelekea beki huyo raia wa Ugiriki kuvunjika mfupa wa bega.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live