Fri, 9 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo Felix Tshisekedi, ameipongeza timu ya Taifa ya DRC kwa hatua ambayo wamefikia kwenye Mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika.
DR Congo imechapwa na Côte d’Ivoire kwenye hatua ya nusu fainali bao 1-0 ambapo ilifika katika hatua hiyo baada ya kuziondoa Misri hatua ya 16 bora na Guinea kwenye robo fainali
Rais Tshisekedi amesema kwa hatua ambayo wamefikia ni heshima kwa nchi pia akiitakia ushindi katika mchezo wa kutafuta nafasi ya tatu dhidi ya Afrika Kusini “Bafana Bafana siku ya Jumamosi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live