Mon, 27 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Beki wa kushoto na Naohodha Msaidizi wa Simba SC, Mohamed Hussein 'Tshabalala' amewataka mashabiki wa Simba SC kuwa kitu kimoja kwenye nyakati hizi ngumu wanazopitia.
Tshabalala amesema kama wachezaji, wanajipanga kwenda kufanya vizuri kwenye mchezo unaofuata dhidi ya Jwaneng Galaxy nchini Botswana.
"Tulitereza lakini tutaamka na kusimama upya. Sisi kama wachezaji tutakwenda kupambana kiume kwenye mchezo unaofuata na ninaamini tutapata matokeo," alisema Tshabalala.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live