Tue, 15 Mar 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
MWENYEKITI wa Bodi ya Wakurugenzi Simba,Salim Abdallah, 'Try Again' amesema kuwa malengo ya timu hiyo ni kufanya vizuri kimataifa.
Machi 13,2022 ubao wa Uwanja wa Mkapa ulisoma Simba 1-0 RS Berkane katika mchezo wa Kombe la Shirikisho hatua ya makundi ikiwa ni kundi D ambalo linaongozwa na Simba yenye pointi 7.
Try Again amesema:"Katika mashindano ya kimataifa tuna uzoefu hatuna mashaka na wachezaji wanajua kwamba tunahitaji ushindi hivyo hilo linafanyiwa kazi katika kila mechi ambayo tunacheza mashabiki wazidi kuwa pamoja nasi, lengo letu ni kufanya vizuri zaidi".
Chanzo: www.tanzaniaweb.live