Mchezaji wa ‘klabu’ ya Arsenal, Leandro Trossard ameondolewa katika kikosi cha ‘timu’ ya Taifa ya Ubelgiji kinachoenda kushiriki michuano ya kufuzu EURO 2024 kutokana na majeraha ya misuli ya paja.
Mchezaji wa ‘klabu’ ya Arsenal, Leandro Trossard ameondolewa katika kikosi cha ‘timu’ ya Taifa ya Ubelgiji kinachoenda kushiriki michuano ya kufuzu EURO 2024 kutokana na majeraha ya misuli ya paja. Leandro Trossard ni majeruhi wa tatu katika ‘klabu’ ya Arsenal ambapo Bukayo Saka na William Saliba nao watalazimika kuwa mapumzikoni kufuatia majeraha yao, hata hivyo mpaka sasa hajajulikana ni kwa muda gani watakuwa nje ya uwanja.