Wed, 15 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Tottenham wamesema hawako tayari kumuuza mshambuliaji wao kutoka nchini Uingereza Harry Kane katika msimu wa joto.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29, mkataba wake na Spurs unakamilika msimu mwaka 2024, huku klabu hiyo ikijipanga kumuongezea mkataba kutokana na uwezo wake katika timu hiyo.
Taarifa kutoka Sky Sports zinadai kuwa kuna uwezekano mkubwa wa Kane kutokusaini mkataba mpya na Spurs.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live