Wed, 22 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nyota wa zamani wa klabu ya Barcelona Jean Clair Todibo ameeleza kipindi kibaya zaidi alichowahi kukutana nacho kwenye soka ni pale alipokosa wa kuongea nae akiwa Barcelona tofauti na Eric Abidal.
"Niliambiwa kuwa naenda kuwa mrithi wa Gerard Pique, lakini sikupata nafasi hiyo."
"Nilicheza mechi tano [5] pekee na nilifanya vizuri tu, lakini hawakuongea chochote, hakuna aliyekuwa anataka kuongea na mimi pale Barcelona tofauti na Eric Abidal pekee." Jean Clair Todibo akielezea maisha yake akiwa Barcelona.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live