Mchambuzi wa soka, Master Tindwa amesema kutokana na ubora wa virabu vya Tanzania, timu za Kaskazini kwa sasa zinakuja kwa adabu.
Tindwa amesema, kwa sasa mpira wa Tanzania umekua na imefika wakati timu kubwa na kongwe Afrika, zinapata wakati mgumu sana kupata matokeo.
"Kwa sasa hizi timu za kaskazini mwa Afrika hasa kutoka Misri sidhani kama wanafurahia kama kwenye ratiba wanakutana na timu za Tanzania, kwa sababu ukiangalia hivi karibuni wanapata tabu sana, wanapata tabu kupata matokeo. Zamani wakisikia timu za Tanzania walikuwa wanadhani ndio sehemu ya kupita, sasa hivi wanaona jasho na damu," alisema Master Tindwa.