Meneja wa habari na Mawasiliano na Simba SC, Ahmed Ally amesema klabu yao inasemwa kuwa ni mbovu lakini wachezaji wake wanaongozwa kwa kutakiwa na vilabu vingine.
Kupitia ukurasa wake wa Instagram, Ahmed ameweka picha ya Kibu Denis akiwa na wachezaji wenzake wa Simba na kushusha ujumbe huo.
"Licha ya timu yetu kusemekana ni mbovu lakini ndio timu inayoongoza kwa wachezaji wake kuhitajika na vilabu vingi zaidi vya ndani na nje nchi
Ni dhahiri kuwa tuna kikosi chenye Wachezaji bora
Hatujapata matokeo mazuri msimu huu lakini haindoi ukweli kuwa wachezaji wetu ni bora sana ndio maana wanatajwa sana sokoni
Tunachoenda kukifanya hivi sasa ni kubaki na wale bora wenye moyo wa kuitumikia Simba
Katika dirisha hili la usajili tunaemtaka atabaki Simba lengo ni kutengeneza Simba tishio turudi kwenye Ufalme wetu."