Fri, 17 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya idara ya masoko na mauzo ya Azam FC, imepata ajali alfajiri ya leo katika eneo la Magunike Dumila mkoani Morogoro, ilipokuwa safarini kuelekea Mwanza ambapo vijana hao wa mitaa ya Chamazi watacheza mchezo wa nusu fainali ya #CRDBBankFederationCup dhidi ya Coastal Union.
Kwa mujibu wa taarifa ya Azam FC, ndani ya gari hilo binafsi kulikuwa na watu watatu, Meneja wa idara, Tunga Ally na wasaidizi wake wawili, Ayubu Shelukindo na Venock Mkisi.
Meneja Tunga Ally aliyekuwa akiendesha, ndiye aliyeathirika lakini wengine waliobaki walitoka salama.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live