Thu, 1 Jun 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya Leicester City kushuka daraja kutoka Ligi kuu England baadhi ya nyota wa klabu hiyo wanaripotiwa kuanza kuondoka klabuni hapo huku kiungo Mbelgiji, Youri Tielemans akiwa mstari wa mbele kuondoka.
Kupitia ukurasa wake wa mitandao ya kijamii, Tielemans amethibitisha habari hizo huku mkataba wake klabuni hapo ukimalizika mwishoni mwa Juni.
"Baada ya miaka 4.5 ya kipekee kwa shukrani nyingi, ninaiaga klabu hii ya ajabu. Tangu siku ya kwanza kuweka mguu kwenye ardhi hii, joto na shauku yenu ilinikumbatia." Ameandika Tielemans
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: