Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Thomas Frank, Enzo Maresca na De Zerbi waongoza kibarua cha kuinoa Chelsea

Thomas Frank, Enzo Maresca Na De Zerbi Waongoza Kibarua Cha Kuinoa Chelsea Thomas Frank, Enzo Maresca na De Zerbi waongoza kibarua cha kuinoa Chelsea

Mon, 27 May 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

SHARE Kieran McKenna hatafikiriwa tena kuchukua nafasi ya Mauricio Pochettino huko Chelsea, huku wagombea watatu sasa wakiwa wamesalia kwenye kinyang’anyiro hicho na uteuzi unatarajiwa wiki hii.

Wagombea hao wakiwa ni Thomas Frank, Enzo Maresca na Roberto De Zerbi, wote watatu wanaonekana kuwa na sifa zinazofaa kwa kazi hiyo.

Orodha hiyo inaakisi nia ya kutaka kumteua kocha mahiri, mwenye fikra za mbele na mwenye maendeleo ambaye anaendana na itikadi za klabu na ambaye ana uzoefu wa kufundisha soka la Uingereza kwa kiwango cha juu.

Kocha mkuu mpya wa Chelsea atatia saini mkataba ambao utakuwa mrefu zaidi ya mkataba wa miaka miwili ambao Pochettino alikubali msimu uliopita wa kiangazi.

Wakurugenzi wenza wa Chelsea Paul Winstanley na Laurence Stewart wamekuwa wakifanya kazi ya kuandaa orodha fupi ya mwisho ya wagombea waliopendekezwa.

Uamuzi wa mwisho kuhusu kocha mkuu mpya utafanywa na kundi la umiliki wa Chelsea, ambalo linajumuisha wamiliki wenza Behdad Eghbali na Todd Boehly.

Wadau waandamizi wa Chelsea wanaamini kuwa kocha mkuu mpya ndiye atakuwa sehemu ya mwisho ya muundo wa kisasa walioujenga katika klabu hiyo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live