Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Thiago Alcantara atundika Daluga

Thiago Alcantara 2.jpeg Thiago Alcantara

Sun, 7 Jul 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Aliyekuwa kiungo wa Barcelona, Bayern Munich, Liverpool na Timu ya taifa ya Uhispania, Thiago Alcantara ameamua kustaafu soka la kulipwa akiwa na umri wa miaka 33.

Thiago ambaye mkataba wake na Liverpool ulitamatika mwishoni mwa msimu uliopita alianza maisha yake ya soka kwenye shule ya kukuza vipaji ya Barcelona almaarufu La Masia na kupandishwa kwenye timu ya wakubwa mnamo Julai 1, 2011.

Mnamo Julai 14, 2013 alijiunga na Bayern Munich ya Ujerumani na kudumu kwa miaka 7 kabla ya kutimkia Liverpool mnamo Septemba 18, 2020.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live