Fri, 18 Aug 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa zamani wa Arsenal, Theo Walcott ametangaza kustaafu soka la kulipwa akiwa na umri wa miaka 34.
Walcott amewahi kuichezea timu ya Taifa England mechi 47 huku akifunga magoli 8.
Kwenye ngazi ya klabu amewahi kuchezea Southampton akatimkia Arsenal na baadae Everton kabla ya kurejea tena Southampton.
Kwa ujumla amecheza mechi 563 kwenye ngazi ya klabu huku akifunga magoli 129.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live