Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tetesi za Usajili Dirisha Dogo 2022/23 Ligi Kuu ya NBC

Ajibu Azam Banch Tetesi za Usajili Dirisha Dogo 2022/23 Ligi Kuu ya NBC

Sun, 11 Dec 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Klabu ya Singida Big Stars FC ya mkoani Singida imefanikiwa kuinasa saini ya kiungo Ibrahim Ajibu “Migomba” kutoka Azam FC Kama mchezaji huru.

Kiungo wa Azam FC, Kenneth Muguna raia wa Kenya anajiandaa kuachana na klabu hiyo yenye makazi yake Jijini Dar es Salaam pindi mkataba wake utakapomalizika mwishoni mwa msimu huu wa 2022/2023. Mguna alijiunga na Azam FC akitokea Gormahia ya kwako Kenya.

Kocha wa zamani wa vilabu vya Dodoma Jiji na Mbeya Kwanza Mbwana Makata anatajwa kuwa mrithi wa Charles Mkwasa “Master” aliyeachana na Ruvu Shooting FC.

Peterson Cruz nyota wa Singida Big Stars FC ameomba kuondoka klabuni hapo ili arejee nyumbani kwao Brazil kwaajili ya kushugulikia masuala yake ya kifamilia

Washambuliaji Shaban Idd Chilunda pamoja, Rogers Cola pamoja na Salula huenda wakaachana na klabu yao ya Azam FC kwenye dirisha hili dogo la Usajili.

Klabu ya Polisi Tanzania FC ya Moshi mkoani Kilimanjaro imeachana na kiungo wake Omary Chibada.

Kiungo huyo wa zamani wa vilabu vya timu ya vijana ya Yanga SC (U-20), Yanga SC na Biashara United hivyo kwa sasa ni mchezaji huru.

Mshambuliaji wa zamani wa Ihefu SC, Erick Msagati hana timu kwa sasa tangu alipoachwa na klabu hiyo huku kuisaidia Ihefu kurejea Ligi Kuu Tanzania Bara (NBC Premier League 2022/2023).

Msagati amewahi kuitumikia timu ya vijana na timu ya wakubwa ya Yanga SC pamoja na Vilabu vya Coastal Union FC, Biashara United FC na Polisi Tanzania FC.

Baada ya kufunga mabao 7 na kutoa Assist 6 msimu huu kwenye NBC Premier League 2022/2023, Mshambuliaji wa Mbeya City FC, Sixtus Sabilo anawindwa na vilabu vya Singida Big Stars pamoja na Klabu yake ya zamani Namungo FC ya Ruangwa mkoani Lindi.

Klabu ya Mashujaa ya mkoani Kigoma inayoshiriki Championship League imeachana na kocha wake Jumanne Chale kutokana na matokeo mabovu.

Pia uongozi wa klabu hiyo umewasimamisha wachezaji wao wanne kwa utovu wa nidhamu, wachezaji hao ni Khamis Thabiti, Said Mwande, John Mbilinyi na Moses Msukanywele. Kwa sasa timu hiyo itakuwa chini ya Kocha msaidizi wa Rashid Idd Chama.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live