Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tetesi za Soka Barani Ulaya, Januari 5

Aubameyang Mshambuliaji wa Arsenal, Pierre-Emerick Aubameyang

Wed, 5 Jan 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Arsenal itapokea ofa ya mshambuliaji wa Gabon Pierre-Emerick Aubameyang, 32, ambaye anaweza kuondoka katika klabu hiyo mwezi huu. (Sky Sports)

Gunners wametangaza ofa ya Euro milioni 70 (Pauni milioni 58.3) kumnunua mshambuliaji wa Fiorentina na Serbia Dusan Vlahovic - hatua ambayo huenda ikamfanya kiungo wa kati wa Uruguay Lucas Torreira, 25, kuhamia klabu hiyo ya Serie A club kwa mkataba wa kudumu. (Gazzetta dello Sport - in Italian)

Mshambuliaji wa Red Bull Salzburg Mjerumani Karim Adeyemi, 19, analengwa na Borussia Dortmund kuchukua nafasi ya mshambuliaji wa Norway Erling Braut Haaland, 21.

Wachezaji wengine walio katika orodha ya na klabu hiyo ni mshambuliaji wa Fiorentina Vlahovic, Mshambuliaji wa Stuttgart na Austria Sasa Kalajdzic, 24, na mshambuliaji wa Benfica na Uruguay wa miaka 22- Darwin Nunez wote kutoka Ligi Kuu ya Ujerumani, maarufu Bundesliga. (Marca - in Spanish)

Borussia Dortmund wanataka hatma ya Haaland kuamuliwa kabla dirisha la uhamisho wa Januari kufungwa. (Mirror)

Mshambuliaji wa Flamengo Mbrazil, Gabriel Barbosa, 25, yuko tayari kujiunga na Newcastle United licha ya klabu hiyo kukabiliwa na tishio la kushushwa daraja. (90min)

Kiungo wa kati wa Uholanzi Donny van de Beek, 24, atatathmini chaguo lake Januari huku mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 24 akifikiria kuondoka Manchester United. (ESPN)

Mkufunzi wa Tottenham Antonio Conte bado hajakutana na mwenyekiti Daniel Levy kujadili uhamisho wa Januari. Kiungo wakati wa AC Milan na Ivory Coast Franck Kessie, 25, ni miongoni mwa wachezaji wanaolengwa na Mtaliano huyo. (Evening Standard)

Klabu za Brighton na Crystal Palace zinapania kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Eddie Nketiah,22, mwezi huu wa Januari. (Sun)

Roma anajiandaa kukamilisha uhamisho wa mkopo wa kiungo wa kati wa Arsenal Ainsley Maitland-Niles, 24, wiki. (ESPN)

Paris St-Germain wanataka kumsajili mshambuliaji wa Barcelona- Ousmane Dembele,24. (Mundo Deportivo - in Spanish)

Barcelona itamuuza Dembele endapo winga huyo atakataa ofa ya mwisho ya kandarasi. (Talksport)

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola yuko tayari kumuachilia mlinzi wa Uhispania Aymeric Laporte, 27, kuondoka katika klabu hiyo na kujiunga na Barcelona - lakini atafanya hivyo ikiwa watafikia mkataba utakaomwezesha kiungo wa kati wa Uholanza Frenkie de Jong, 24, kuhamia klabu hiyo ya Ligi ya Primia. (El Nacional, via Teamtalk)

Mshambuliaji wa Italia Lorenzo Insigne atajiunga na klabu ya MLS ya Toronto msimu wa joto baada ya nahodha huyo wa Napoli mwenye umri wa miaka 30 kukubali mshahara wa euro milioni 11. (Guardian)

Chanzo: www.tanzaniaweb.live