Thu, 18 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Unaambiwa Mshambuliaji wa Manchester United Anthony Martial ameambiwa afanye mazoezi peke yake ili kuboresha utimamu wake kabla ya Erik Ten Hag kufikiria kumchagua kwa ajili ya mechi zijazo za klabu hiyo.
Ten Hag anaamini kuwa Martial haonekani kuwa fiti vya kutosha kwa ajili ya kufanya kazi na kikosi cha kwanza kutokana na kiwango chake mazoezini kushuka.
Je, unadhani kitendo hiki cha kutenga wachezaji kinasaidia kuijenga timu au kinaibomoa timu?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live