Thu, 5 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Man United, Mdachi Erik Ten Hag amemtetea mlinda mlango wake Andre Onana licha ya kufanya makosa katika mchezo wa Ligi ya Mabingwa dhidi ya Galatasaray siku ya Jumanne.
Mchezo huo ulioisha kwa Man United kukubali kipigo cha mabao 3-2 katika Dimba la Old Trafford.
Akizungumza Ten hag anasema;
“Nitamtia moyo Onana, nitamfanya arudi sawa— nitamuunga mkono. Ni kipa mzuri. Anaweza kuwa mmoja wa Magolikipa bora duniani.Tayari tumeshawahi kuona uwezo mkubwa wa Onana na pia haiba yake. Atarudi tena kwenye ubora wake,nina uhakika."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live