Fri, 17 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Klabu ya Real Madrid C.F. raia wa Ufaransa Auriliém Tchouméni amekutwa hana chembechembe zozote za kumuonesha kuwa anatumia madawa ya kuongeza nguvu.
Mamlaka za nchini Ujerumani zilimuweka kizuizini mchezaji huyo mara baada ya Mchezo wa nusu fainali dhidi Bayern München kwa kuhisiwa kuwa anajihusisha na utumiaji wa madawa ya kuongeza nguvu michezoni.
Baada ya uchunguzi kukamilika sasa ni rasmi kiungo huyo atajumuishwa katika kikosi kitakachotumika kwenye mchezo wa Fainali ya UEFA Champions League dhidi ya Borussia Dortmund tarehe 1st June 2024.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live