Mashabiki wa Simba Sports Club wamejazana katika Uwanja wa ndege Mkoani Tabora, wakiisubiri timu hiyo ambapo itakipiga na KMC katika dimba la Ali Hassan Mwinyi.
Simba ambayo ilishindwa kucheza mchezo wake uliopita baada ya idadi kubwa ya wachezaji wake kukumbwa na ugonjwa, watakuwa wageni katika mchezo huo.
Tazama mbwembwe za mashabiki nje ya Uwanja;
KMC vs SIMBA: Mashabiki wa simba wakiwa uwanja wa ndege wa Tabora wakiisubiri timu yao kutua mkoani humo kuivaa KMC
— Azam TV (@azamtvtz) December 22, 2021
Disemba 24, vijana wa Manispaa ya Kinondoni, watavaana na Simba SC dimbani Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora.#AzamSports1HD #NBCPremierLeague #NBCPL pic.twitter.com/AiblmBt4iz