Nyota wa zamani wa soka nchini Salehe Zimbwe (Farasi Mweupe) amefariki jana usiku katika hospitali ya Ngamiani Tanga.
Zimbwe aliwika sana wakati wa enzi zake akiwa na ndogo wake Omar Zimbwe kwenye miaka ya 1960 na 1970 hasa akichezea timu yake ya African Sports ya Tanga kwenye michuano maarufu enzi hizo ya Sunligt na Taifa Cup pamoja pia kuichezea timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars.
Marehemu Zimbwe alifanyiwa huku Operesheni ya tezi dume iliyofaulu alirejea Tanga kiiasi cha wiki 2 zikizopita lakini jana inaelezwa hali yake illibadikika ghafla ambapo alifariki kwenye hospiitali ya Ngamiani wakati anapatiwa matibabu.
Pumzika kwa amani Gwiji la soka la zamani la Tanzania Saleh Zimbwe ‘Farasi Mweupe’.