Wed, 1 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Nguli wa soka wa Ufaransa na kocha wa zamani wa Paris Saint German kati ya mwaka 1973-76, Just Fontaine amefariki Dunia akiwa na umri wa miaka 89.
Fontaine bado anashikilia rekodi mfungaji wa mabao mengi (13) zaidi kwenye toleo moja la kombe la Dunia ambapo alifunga magoli 13 kwenye mechi 6 mnamo 1958.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live