Sat, 30 Oct 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Tanzania imeanza vyema michuano ya wasichana chini ya umri wa miaka 20 Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Challenge Women’s 20 baada ya kuichapa Eritrea 1-0 jioni ya leo Uwanja wa FTC Njeru nchini Uganda.
Bao pekee la Tanzanite jioni ya leo limefungwa na Clara Luvanga dakika ya 90 na timu hiyo itashuka tena dimbani Jumatatu kumenyana na Burundi.
Siku ya Jumatano itashuka uwanjani kuivaa Ethiopia, Uganda Jumamosi ijayo na kukamilisha mechi zake kwa kucheza na Djibouti Novemba 9.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live