Sat, 20 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Tanzania imefanikiwa kuingia fainali michuano ya COSAFA Soka la Ufukweni baada ya ushindi wa 5-2 dhidi ya Angola leo ufukwe wa South Beach Arena Jijini Durban, Afrika Kusini.
Katika mechi hiyo, mchezaji wa Tanzania, Stephano Manyama amechaguliwa kuwa mchezaji bora wa mchezo huo na sasa timu hiyo iliyopo chini ya kocha Boniphace Pawasa itakutana na Msumbiji katika fainali Jumapili.
Msumbiji ambayo iliifunga Tanzania kwa penalti 4-3 baada ya sare ya 4-4 katika mchezo wa Kundi B jana, leo imewafunga wenyeji, Afrika Kusini 5-3 katika Nusu Fainali nyingine.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live