Wed, 3 Nov 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Timu ya Taifa ya Wanawake chini ya miaka 20,"Tanzanite" imechapwa 2-1 na Ethiopia katika mfululizo michuano ya CECAFA wanawake U20 mchana wa leo Uwanja wa FTC Njeru nchini Uganda.
Kipigo hicho kinakuja baada ya Tanzanite kushinda mechi mbili za awali, 1-0 dhidi ya Eritrea na 3-2 dhidi ya Burundi.
Tanzanite itashuka tena dimbani Jumamosi kuivaa Uganda kabla ya kukamilisha mechi zake kwa kucheza na Djibouti Novemba 9.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live