Tangu mwaka 2024 umeingia, Singida Fountain Gate FC haijashinda mchezo wowote wa Ligi Kuu! Katika michezo saba [7] ambayo imecheza mwaka huu, imetoka sare michezo mitatu na kupoteza michezo minne.
Michezo ya Ligi Kuu ya Singida kwa mwaka 2024;
- Singida 2-2 JKT Tanzania
- Singida 0-0 KMC FC
❌ Geita Gold 1-0 Singida
❌ Kagera Sugar 1-0 Singida
❌ Tanzania Prisons 3-1 Singida
- Tabora United 1-1 Singida
❌ Singida 0-1 Azam FC.
Mara ya mwisho Singida Fountain Gate FC kupata ushindi kwenye mchezo wa Ligi Kuu ilikuwa ni Novemba 27, 2023 iliposhinda 2-1 dhidi ya Coastal Union. Singida Fountain Gate FC ipo nafasi ya nane kwenye msimamo wa Ligi ikiwa na alama 21.