Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Tambwe arejea soka la Bongo

Amissi Tambwe Yanga 1poj3lxpqevvb1ux8s2nc4zc5m.png Aliekua Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe

Tue, 17 Aug 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

DTB FC inayoshiriki Ligi Daraja la Kwanza, imethibitisha nia yao ya kumrudisha nchini straika maarufu Mrundi, Amissi Tambwe.

Tambwe aliyewahi kucheza katika klabu za Simba na Yanga anasifika kwa utupiaji nyavuni na Katibu Mkuu wa DTB, Muhibu Kanu amesema; “Ni kweli tuko kwenye mazungumzo, tukikubaliana atakuja.”

Habari za uhakika kutoka kwa mtu wa karibu na mchezaji huyo alilidokeza Mwanaspoti kwamba Tambwe anarejea nchini wakati wowote kuanzia jana baada ya kumalizana kila kitu na mmoja wa vigogo wa timu hiyo.

“Tambwe anarejea nchini kuanzia wiki hii, ameshaelewana kila kitu na bosi wa timu hiyo na anakuja kusaini mkataba, ameamua kuja huku kwa sababu ameona timu hiyo inajipanga kupanda Ligi Kuu,” kimesema chanzo hicho.

Wakati huo huo, inaelezwa vigogo wa klabu hiyo wapo kwenye mipango ya kumrejesha nchini Tafadzwa Kutinyu, raia wa Zimbabwe aliyewahi kucheza Singida United na Azam FC.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz