Thu, 9 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Simba SC inashuka dimbani leo kwenye uwanja wake wa nyumbani kuwakabili Namungo FC mchezo wa raundi ya tisa ya Ligi Kuu ya NBC.
Kuelekea mchezo huo, takwimu zinaibeba zaidi Simba kuliko Namungo kwani katika michezo tisa iliyopita katika mashindano yote waliyokutana, ushindi mkubwa wa Namungo ni sare.
Namungo wamepata sare 3, wamefungwa 6 na wao hawajashinda hata mchezo mmoja.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live