Achana na kununua tiketi zote za viti vya mzunguko na kuzigawa bure kwa mashabiki watakaokuwa wamevalia jezi za Yanga, Mwanaspoti limepenyezewa mdhamini wa timu hiyo, Gharib Said Mohamed amewaahidi mkwanja mrefu wachezaji wa Yanga kama watashinda mechi hiyo.
Licha ya uongozi wa Yanga kushindwa kuweka wazi ni kiasi gani watavuna kutoka kwa GSM kama watashinda, lakini hadi tunaingia mitamboni ilikuwa ikifahamika si chini ya Sh300 milioni.
Huo umekuwa utaratibu wa GSM tangu aanze kuipa sapoti timu hiyo na mara ya mwisho kutoa mkwanja mrefu ni pale chama lake lilipoichapa Simba mabao 5-1 kumbuka ni tofauti na ile ambayo inatolewa na Yanga.