Timu ya Taifa ya Tanzania (Taifa Stars) imehitimisha mapumziko ya kimataifa kwa ushindi mnono wa 3-0 dhidi ya Mongolia katika mchezo wa FIFA Series 2024 huko Baku, Azerbaijan
FT: Tanzania 3-0 Mongolia
⚽ Kelvin John 49’
⚽ Abdul Sopu 63’
⚽ Novatus Miroshi 76’.
Mchezo huo umemaliza jioni hii katika uwanja wa Liv Bona Dea Arena katika Mji wa Baku nchini Azerbaijan.
Waliofunga Magoli ya Taifa Stars leo dhidi ya Mongolia; Kelvin John umri wa miaka 20, Novatus Miroshi miaka 21 na Abdul Sopu miaka 22. Hakika kesho ya Taifa Stars na vijana hawa itakuwa bora zaidi.
Je, ni wakati sasa wa kuwaamini vijana kwenye timu ya Taifa?