Mon, 16 Oct 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa Timu ya Taifa ya Sudan, James Appiah amesema, Tanzania sio nchi ndogo kwenye mpira, ina wachezaji wazuri lakini wana changamoto kwenye eneo la ufungaji.
Appiah amefunguka hilo jana mara baada ya kumalizika kwa mchezo wao wa kirafiki na kutoka sare ya 1-1.
"Tanzania (Taifa Stars) walicheza vizuri sana hususan kipindi cha kwanza, kipindi cha pili Sudan walirudi mchezoni na kucheza vizuri. Tanzania sio nchi ndogo kimpira, wamecheza vizuri, wamelinda vizuri lakini wana tatizo kwenye ufungaji," alisema kocha huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live