Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Taifa Stars kunoa makali ya kuiua Sudan kwa Rwanda

78337 Stars+pic

Thu, 3 Oct 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’ itacheza mechi ya kirafiki na Rwanda Oktoba 14 siku nne kabla ya kuivaa Sudan katika mchezo wa kusaka kufuzu kwa fainali za CHAN2020 Cameroon.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) mchana huu inasema Taifa Stars imepata mechi ya kirafiki dhidi ya Rwanda 'The Amavubi' mchezo uliopangwa kufanyika Oktoba 14 jijini Kigali Rwanda.

Mchezo huo utakuwa ni mchezo wa kwanza kwa Stars wa kirafiki katika utawala wa makocha wawili tofauti tangu Mnigeria Emmanuel Amunike mpaka sasa kaimu kocha  Mrundi Ettiene Ndayiragije haikuwahi kupata mchezo wa kirafiki.

Mapema kabla ya kutimuliwa Amunike aliwasilisha changamoto kubwa ya timu hiyo kukosa mechi za kujipima nguvu ambapo fursa hiyo imekuwa ikikwamisha makocha kuweza kuwapima wachezaji wao.

TFF imesema mchezo huo dhidi ya Rwanda utakuwa ni katika kalenda ya Shirikisho la Soka Duniani (FIFA).

Aidha TFF imethibitisha kuwa mchezo wa kikosi cha timu hiyo kwa wachezaji wa ndani kuwania kucheza Fainali cha CHAN sasa utapigwa jijini Omdurman katika Uwanja wa El Merreikh.

Pia Soma

Advertisement
Mchezo huo utachezeshwa na waamuzi kutoka Burundi ambapo Stars inahitaji ushindi kuweza kufuzu fainali hizo zitakazofanyika mwakani nchini Cameroon wakiwa na kumbukumbu ya kipigo cha bao 1-0 kutoka kwa Sudan katika mchezo wa kwanza uliofanyika nchini wiki moja na nusu iliyopita.

Waamuzi hao watakuwa ni Thierry Nkuruzinza atakayekuwa mwamuzi wa kati akisaidiwa na mwamuzi msaidizi wa kwanza Willy Habimana na mwamuzi wa pili msaidizi akiwa Shabani Niyungeko wakati mwamuzi wa akiba akiwa Georges Gatogato

Chanzo: mwananchi.co.tz