Andiko la leo linawahusu nyota ambao wameshikilia kesho ya soka la nchi yetu lakini ambao bado wanakiwasha hapa hapa kwenye ligi ya nyumbani.
Wapo baadhi ambao nafasi zao vikosini zimekuwa finyu lakini kila wakipata nafasi unaona kuwa wanayo hiyo talent kubwa ila wanachohitaji ni makuzi sahihi ili nchi ije ifaidi vipaji vyao.
Hawa hapa baadhi ya nyota ambao bado ni vijana wadogo lakini tayari wanaonekana kukua siku baada ya siku.
Raheem Shomari- KMC FC
Pascal Msindo- Azam FC
Ladack Chasambi- Simba SC
Shekhan Hamis- Yanga SC
Zidane Serili- Dodoma Jiji
Lameck Lawi- Coastal Union
Yona Amos- Tanzania Prisons
Samson Mwaituka- Tanzania Prisons.
Hawa ni baadhi tu lakini wapo wengi ambao wanahitaji kupata nafasi ya kukua na kuonyesha uwezo wao.
Hii ni kwa faida ya soka letu kesho na keshokutwa.
Nani unamuona akiwa na “carrier” bora sana.