Wed, 17 Jan 2024
Chanzo: Mwanaspoti
Tabora United imekwama dakika za mwisho kumchukua kiungo mshambuliaji Joseph Akandwanaho aliyekuwa Mlandege ya Zambia kwa muda.
Tabora ikiwa inakaribia kukamilisha kila kitu klabu ya Mbarara City ya Uganda yenye mkataba na kiungo huyo imetuma barua Kali ya kisheria kwa Mlandege ikitaka kufahamu sababu za kumvalisha jezi za Mabingwa hao wa Kombe la Mapinduzi.
Akandwanaho ana mkataba wa mwaka mmoja na Mbarara ambapo hatua hiyo imeifanya Tabora kurudi nyuma na kusitisha mpango wao huo.
Chanzo: Mwanaspoti