Fri, 10 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Shirikisho la mpira wa Miguu Tanzania (TFF), limetoa tahadhari kwa vilabu na makocha kuhusiana na kupata leseni za kufundisha Mpira wa miguu nchini Tanzania.
Katika taarifa yake TFF, imesema hakuna Kocha atakaeruhusiwa kukaa kwenye benchi bila kuwa na Lesni inayotambuliwa ama kutolewa na shirikisho hilo.
Kwa sasa Fomu za maombi ya leseni zinapatikana katika tovuti ya TFF.
Sehemu ya taarifa ya TFF
Chanzo: www.tanzaniaweb.live