Wed, 8 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
TP Mazembe imekubali kipigo cha pili mfululizo dhidi ya US Monastir ikiwa ni kipigo cha tatu mfululizo kwenye hatua ya makundi ya kombe la Shirikisho Afrika.
Mazembe ambayo ipo kundi D sambamba na Timu za US Monastir, Yanga na Bamako mpaka sasa imecheza michezo minne na kukusanya alama tatu pekee.
Mazingira yanazidi kuwa magumu kwa Mazembe kupenya hatua ya Robo Fainali ya Michuano hiyo baada ya leo Machi 8 kukubali kipigo cha bao 1-0.
MSIMAMO KUNDI D
Us Monastir 10
Yanga SC 4
TP Mazembe 3
Real Bamako 2
Yanga na Real Bamako wapo Uwanjani muda huu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live